Uganda: Mwanamke apigwa na Kunyeshwa sumu Baada ya kuwa Mkristo

2 years ago By Nyimbo Mpya 541
Are you a music lover looking for the latest track to add to your playlist? Look no further. Get ready for an unforgettable musical experience as we present a song by Uganda: Mwanamke apigwa na Kunyeshwa sumu Baada ya kuwa Mkristo.

Uganda: Mwanamke apigwa na Kunyeshwa sumu Baada ya kuwa Mkristo


Mwanamke mmoja mashariki mwa Uganda, ambaye hivi karibuni amebadili dini na kuwa mkristo amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya baba yake na ndugu zake wenye msimamo mkali kumshambulia na kumlazimisha kunywa sumu.

Hajat Habiiba Namuwaya, 38, alikimbia nyumbani kwake katika kijiji cha Namakoko na kukimbilia nyumbani kwa mchungaji wake baada ya kugundua kuwa baba yake alikuwa anamtafuta.

“Mama yangu alinionya kuwa familia ilikuwa inapanga kuniua,” Namuwaya aliiambia Morning Star News akiwa kitandani kwake hospitalini. “Nilieleza hofu yangu kwa mchungaji, na mchungaji pamoja na familia yake walikubali kunikaribisha, na kwa uhuru nilishiriki wazi maisha yangu mapya katika Kristo na marafiki kwenye WhatsApp, ambayo iliniingiza matatani.”

Mnamo Juni 20, alikutana na baba yake na ndugu wenye hasira ambao walianza kumpiga.

“Alianza kunipiga na kunitesa kwa kitu butu, akinipa michubuko mgongoni, kifuani, na miguuni, na mwishowe alinilazimisha kunywa sumu, ambayo nilijaribu kuikataa lakini nikameza kidogo,” Namuwaya alielezea.

Majirani walisikia kilio chake cha kuomba msaada na hapo ndipo ndugu hao waliondoka eneo la tukio.

“Mchungaji hakuwa karibu wakati washambuliaji walipofika, lakini jirani yake alimpigia simu,” Namuwaya alisema. “Aliogopa kuja haraka lakini baadaye alikuja na kunikuta nikipigania maisha yangu. Nilikimbizwa zahanati ya karibu kupata huduma ya kwanza, na baadaye nikapelekwa mahali pengine kwa matibabu na maombi.”

Watoto wa Namuwaya, wa miaka 5, 7, na 12, wanaishi na baba yao, wakati anaendelea kupona kutokana na majeraha yake. “Sina utulivu na maumivu yanayoendelea ndani ya tumbo langu,” alisema.

Mpaka sasa Namuwaya hajaripoti tukio hilo kwa polisi kwa kuhofia kwamba familia yake italipiza kisasi na kutoa mashtaka ya uwongo dhidi yake.

Namuwaya alihamisha imani yake kwa Yesu Kristo mnamo Februari 24 baada ya kuponywa na saratani ya matiti kufuatia maombi kutoka kwa mchungaji wake.

Habari za CBN ziliripoti mwezi uliopita kwamba mchungaji mwenye umri wa miaka 70 aliuawa nchini Uganda baada ya kundi la Waislamu wenye msimamo mkali kumzuia yeye na mkewe wakati wa kurudi nyumbani kutoka sokoni.

Mapema mwaka huu, umati wa Waislam wenye msimamo mkali walimuua mtu mmoja nchini Uganda wiki moja baada ya kusilimu.

Na Septemba iliyopita, msichana Mkristo wa miaka 13, na kaka yake wa miaka 11 waliripotiwa kutekwa nyara na mwanamke mwenye msimamo mkali wa Kiislam na kuuzwa kwa mganga wa kienyeji kwa kafara ya ibada.

Chanzo: CBN

Download Now 541
Install Android App
Developer: Tanzania Tech Media
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot