SAMIA AELEZA SABABU TAASISI ZA DINI KUTOZWA KODI

2 years ago By Nyimbo Mpya 621
Are you a music lover looking for the latest track to add to your playlist? Look no further. Get ready for an unforgettable musical experience as we present a song by SAMIA AELEZA SABABU TAASISI ZA DINI KUTOZWA KODI.

SAMIA AELEZA SABABU TAASISI ZA DINI KUTOZWA KODI


Rais wa Tanzania, Samia Suluhu ameeleza kuwa Serikali inazitoza kodi taasisi za dini zinazotoa huduma za afya na elimu kwa sababu baadhi zinafanya biashara na si kutoa huduma.

Rais Samia ameeleza hayo leo Alhamisi Julai 8, 2021 wakatia akifungua mkutano mkuu wa 31 wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) unaofanyika mkoani Morogoro.

Amesema wakati mwingine Serikali inakuwa na hospitali na taasisi ya dini inajenga kituo cha afya kwenye eneo hilohilo.

“Hapa ndipo panapokuja lile suala linalolalamikiwa la ushindani wa huduma, taasisi ya dini ina hospitali yake hapo Serikali inajenga kituo cha afya hapo kwa kuona wananchi wakienda huku wanatoa pesa nyingi zaidi kuliko wakipata huduma serikalini.”

“Pia inafanya Serikali kufanya vitu mara mbilimbili kwa kuweka huduma ileile inayopatikana kwa kuweka sehemu moja ambayo sio mtindo mzuri,” amesema

Amesema lengo la Serikali ni kupunguza ugumu wa maisha kwa wananchi ambapo suluhisho lake ni kufanya kazi kwa uwazi na kuaminiana ili wanaotoza kodi wajue taasisi za dini hazifanyi kazi kibiashara.

“Ni lazima mahesabu yawe wazi, watoza kodi waweze kukagua na wajue hali halisi inavyokwenda katika taasisi hizo, ni kweli kumetokea shida mbili tatu katika mifumo hii kuna shule zinazopata misaada kutoka nje, wanapokea wanatoa huduma ya elimu au afya lakini bado taasisi zetu za kodi zimeenda kutoza kodi,”

“Hapa utaona wale wamekusanya jasho la watu wengine sisi tunaenda kutoza kodi, haya yote ni kwa sababu hatukuwa na uwazi, niombe sasa tufanye kazi kwa uwazi na kuaminiana,” amesema.

Rais Samia pia ameeleza kuwa huduma za afya na elimu zimekuwa zikitolewa na sekta binafsi ambapo gharama zinazotolewa kwenye elimu na afya zinalingana ndio sababu na taasisi za dini zikaonekana zinafanya biashara.

“Wale wanaofanya kwenye sekta binafsi malipo yao na viwango ni vilevile vinavyotozwa na taasisi za dini,” ameeleza.

Chanzo: Mwanachi

Download Now 621
Install Android App
Developer: Tanzania Tech Media
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot