Paroko Afunguka Mazito Msiba wa Meya Shinyanga
PAROKO wa Kanisa la Romani Katoliki Ngokolo Mjini Shinyanga Aldof Makandagu, amekemea tabia kwa baadhi ya wanasiasa kutopendana wao kwa wao, kuwa wanafiki, huku wakiuana kwa kusemana maneno hovyo usiku na mchana, na njia zingine zisizoeleweka.
Makandagu amebainisha hayo Jana wakati akitoa Mahubiri kwenye misa ya kumuombea marehemu David Nkulila (57) aliyekuwa Meya wa Manispaa ya Shinyanga.
Amesema hakuna watu wanafiki kama wanasiasa, ambao hupendana kwenye majukwaa tu, lakini wakitoka hapo hakuna upendo na kuanza kunafikiana, huku wakisemana maneno mabaya, na kuwataka waachane na tabia hizo bali wapendane muda wote na siyo kuishi kinafki.
“Kwenye msiba huu Sura zenu hapa zinaonekana zina huzuni, lakini ndani ya mioyo yenu mnachekelea, hizo ndiyo tabia za wanasiasa, hebu jaribuni kupendana muda wote, na kifo hiki kiwe kama funzo kwenu,”alisema Paroko Makandagu
Chanzo: IPP